Social Share Icons

 


Majira ya asubuhi ya  leo March 16 kumetokea tukio la moto kwenye bweni la wanafunzi wa chuo kikuu cha Dar es Salaam.


Kwa mujibu wa kiongozi wa kikosi cha zima moto Kinondoni, Juma Lundawa amesema kuwa chanzo cha ajali hiyo ya moto imetokana na shoti ya umeme kwenye bweni la wasichana (Block B) katika chumba ambacho kinatumiwa kuhifadhi magodoro ya wanafunzi.



Wanafunzi walioshuhudia moto huo wamesema moto ulianza majira ya saa mbili asubuhi huku jitihada za kuuzima moto huo zikiendelea mpaka kikosi cha zimamoto kilipofika kuudhibiti moto huo.



Majeruhi wa tukio hilo ni wanafunzi wawili ambao wamepelekwa katika hospital ya Muhimbili kupata huduma ya matibabu.


 





Soma Nafasi za kazi na ajira bofya hapa chini kutizama, Mjulishe na mwenzio

Facebook Blogger Plugin by Bongo na Matukio

Chapisha Maoni

 
Top